Bukobawadau

Sakata la Rada Tanzania yavutana na BAE ya Uingereza

Mahakama ya Uingereza iliamua juu ya ku Kampuni ya BAE SYSTEM kulipa faini ya dola za marekani milioni 60,kwa serikali ya Tanzania kutokana na udanganyifu uliofanyika katika biashara ya Rada.
Picha ya antena ya rada
Kutokana na hari hiyo kampuni ya BAE imekubari kulipa dola milioni 50 kama hisani kwa Watanzani na ikasema ni haitatoa fedha hizo kwa serikali ya Tanzania bali itazikamizi kwa mashirika ya asasi zisizo za serikali ili ziweze kusimamia vyema ili kila Mtanzania aweze kunufaika kwa njia moja ama nyingine.Na ndipo viongozi wetu wa serikali wakazua mjadara mkubwa na mvutano baina ya kampuni hiyo.
Biashara nyingine ilio wahi kufanywa na kampuni ya BAE ni pamoja na nyambizi kama inavyo onekane katika picha.
Ndege ya kampuni ya BAE ilivyo safirisha Rada

Waziri wa wambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mh.Benardi Membe amesema watanzania ndio tulio ibiwa ivyo basi ni lazima fedha hizo zikabidhiwe mikononi mwa serikali ,kitendo cha kampuni ya BEA Kusema itakabidhi fedha hizo kwa asasi zisizo za kiserikali,inalenga kuionyesha Uingereza kuwa Tanzania haifai na aihaminiki,na imejaa ufisadi.Wakati serikali imeisha panga ikipata pesa hizo ni kujenga nyumba za walimu nchi nzima,kujenga vyoo mashuleni,kununua vitabu na madawati kila wilaya nchi nzima!!!Huku akiongea kwa amasa kubwa na msisitizo mh. Membe amekatoa changamoto kwamba hata shirika litakalo kabidhiwa pesa hizo alitaruhusiwa kuingia nchini na kufanya kazi.

Tunategea na tunaomba maoni yako juu ya sakata hili ndg. mdau kupitia hapa kwenye blog yetu waweza kusema pesa hizo ambazo zilishaibiwa na maofisa wachache katika serikali yetu zikabidhiwe wapi? by mc.
Next Post Previous Post
Bukobawadau