Bukobawadau

TUNATOA PONGEZI KWA MDAU MPAMBANAJI SUNDAY MTAYOBA KWA HATUA HII ALIYOFIKIA

Bukobawadau Blog tunachukua fulsa hii kutoa pongezi zetu za dhati kwa wadau wapambanaji wamiliki wa jengo hili lililopo barabara ya One way mtaa wa  Haki ndani ya manispaa ya mji wa Bukoba,Ikumbukwe ni Jengo lililo kuwa lillilo kuwa limeungua na kuteketea kwa moto na kusababisha asara kubwa ya Mamilion.
Ni jengo ambalo kipindi cha nyuma lilionekana la kihistori kabisa kabla ya umiliki wa wadau hawa Mr Sunday, Mtayoba na Mlangira Gosbert,ambao ni wadau maarufu kwa ukanda huu na wafanya biashara wa kitambo.Kupitia uzoefu wetu kimazingira bukobawadau blog tunapenda kumkumbuka pia mmiliki wa kwanza wa eneo hili ili mpaka  miaka ya 80 Mzee wetu Marehemu Petro Nshange maarufu kama Mzee (PetroTumbo) hii ni katika kile tunacho amini sisi ni moja ya njia ya kuwaenzi wadau waliotangulia mbele haki kwa kuzingatia neno WADAU.
Hivi sasa tayari wadau wanaendelea na biashara zao ambapo wahanga wa ajali ya moto ndio waliopewa kipaumbele kufuatia  utaratibu na ustarabu wa wamiliki,ili nalo ni swala la kiungwana sana.
 Muonekano wa vyumba vya maduka katika jengo hili kwa upande wa pili

Baadhi ya maduka yakiwa yameanza kufanya kazi kama yanavyoonekana  katika picha





Mdau Mlangira Mtayoba mmoja wa wamiliki wa Jengo hili
Mtaa wa Haki barabara ya (one way )ndipo lilipo jengo hili,ni  mtaa wa kibiashara wenye maduka yenye bidhaa mbalimbali
BUKOBAWADAU TUNATOA PONGEZI KWA MDAU MPAMBANAJI SUNDAY MTAYOBA  KWA HATUA HII ALIYOFIKIA

MUHIMU;PITIA OLDER POST KUPATA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE NA MENGINE MENGI.
Next Post Previous Post
Bukobawadau