Bukobawadau

Chama Cha Mapinduzi (CCM) - California chatoa pole kwa waliokumbwa na maafa ya poromoko la jengo la ghorofa mjini Dar-Es-Salaam


CCM Shina la California,Linapenda kutoa salama za pole kwa familia ya ndugu jamaa na marafiki  waliopoteza maisha kutokana na maafa ya kuanguka kwa jengo la ghorofa siku ya tarehe 29 mwezi mwezi wa tatu mwaka 2013. Salamu za pole ziwaendee wale wote waliojeruhiwa na kupelekwa mahospitali, tunaendelea kuwaombea na tunawatakiwa uponaji wa haraka. Halikadhalika na wale pia  walioharibiwa mali zao, nao tunawapa pole.

Msiba huu ni wakitaifa na umetugusa sana na hasa ukizingatia kwamba umakini na uhakiki katika shughuli za kujenga jengo hili haukuwa yakinifu.

Tunatoa shukrani za pongezi kwa Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa hatua za awali za kutaka wale wote waliohusika kuanzia hatua za awali zilizotumika kuandaa shughuli za ujenzi huu mpaka siku lilipoanguka wafikishwe kwenye vyomba vya dola na sheria ichukue mkondo wake. Kauli ya mheshimiwa Rais imetutia moyo na tuna matumaini itatekelezwa kwa vitendo ili liwe funzo kwa wengine.

Lakini pia tuko pamoja na wizara ya Ardhi chini ya Waziri Mheshimiwa Anna Tibaijuka kuwa majengo yote ya ghorofa yanayoendelea kujengwa na yaliyomalizika na yaliyopo maeneo hayo yavunjwe mara moja kwani kuna kila dalili kwamba hayako kwenye viwango bora vinavyotakiwa na yanaweza kuleta madhara kama haya. Kauli ya mheshimiwa waziri imetutia moyo na tuna matumaini kuwa itatekelezwa kwa haraka kuliko kusubiri na kujikuta tunapata janga jingine. Na wahusika wote wawajibishwe ili liwe funzo kwa wengine.

Itakuwa si sahihi kama hatujatoa pongezi zetu za dhati kwa waokoaji kutoka watu binafsi na pia mashirika mbali mbali likiwemo jeshi letu. Ule umoja ulioonyeshwa pale ulitutia moyo wa upendo ingawa pia tumejifunza kwamba nyenzo zaidi katika maafa ya namna hii zinahitajika. Ni matumaini yetu kuwa serikali nalo imeliona hili.

Tunaungana na wananchi wote wa Tanzania katika masikitiko haya, na mategemeo yetu ni kuwa tufanye kazi na jitihada thabiti kwa pamoja kuhakikisha yaliyoahidiwa kudhibiti masuala kama haya yanafanyika kwa vitendo.

ERICK BYORWANGO

KATIBU-SHINA LA CCM CALIFORNIA-USA.
Next Post Previous Post
Bukobawadau