Bukobawadau

SHEREHE YA KUMUAGA BI RAYAH KORONA MUSSA YAFANA ILE MBAYA NDANI YA KISIMA CHA BURUDANI LINAS NIGHT CLUB

Hahahahahahahaha watcha weee wanamelemeta maharusi wetu usiku huu ni Shughuli ya Send off party ya Bi Rahay Mussa na Mdau Mohammed Kassim ndani ya ukumbi wa Linas Club
 Kushoto ni mama mzazi wa Bi Harusi.
 Bi Rukia Kassim , Pichani kulia ambaye ni wifi wa Bi harusi akisema safi shughuli imepamba!!
Mawifi pichani anaonekana Mai katikati na Sister Du Mwaza wakiwa tayari kumpokea wifi yao.
 Mpambe wa Bwana harusi anavibweka usiombe aisee kwa jina anaitwa Mdau Evody Chinga aka Veterani Mkigoma.
Moja ya sifa ya mwanaume ni pamoja na kula kama anavyo onekana Mdau Evody akifanya yake.
Kama vile Bi Harusi wetu, Bi Kolona anasema; 'Mpenzi si tuondoke tu tuwaache wageni waendelee na shughuli!!! hii yote ni ishala ya 'ENGONZI, ebigonzo aka  Upendo.
 Kushoto ni Dada Jane  wa MTK na kulia ni Dada Lilian Peter Mwise,akiongea na Bukobawadau, Bi Jane amesema amekuja kutazama send off hii ili akajipange zaidi siku ya ndoa yenyewe, siku ya Jumamosi tarehe 13 anadai siku hiyo Mtoto hatumwi dukani, kikubwa zaidi bukobawadau tutakuwepo ukumbini hapo live bila kokoro wala zengwe tukirusha hewani tukio zima.
 Wanandugu wa familia kutoka nchi jirani za Uganda na Congo.
Kulikoni Home Boy Moa Kassim, kama vile wanaogopana au ni macho ya Camera yetu!!!
Katika kujiongeza anaonekana Mdau Mbishi Jerry.
 Hili ndilo pozi la mpambe wa Bibi Harusi, hakika hayupo nyuma kabisa.
 Katikati akiwa na tabasamu ni Kaka wa familia Mdau Jamal Kalumuna aka JK.
 Wasiliana na Bukobawadau kupitia 0715 505043,0754 505043au 0784 505045 viber pia tunapatikana BBM kwa pin 234E5 DD7 au 0713 397241 Email bukobawadau@ gmail.com kwetu sisi kazi ndio msingi,Uzalendo ndio sera.
 Dada Oliver nae alikuwepo pia
 Mdau mama Manka.
 TIMU NZIMA YA BUKOBAWADAU BLOG Tunawapongeza maharusi haWA kwa uamuzi wao, wengi wamekuwa wakikwepa kufunga ndoa si kwa kigezo cha imani, bali eti uchumi mdogo!!.

Next Post Previous Post
Bukobawadau