Bukobawadau

Waganga Mkoani KAGERA watakiwa kuzingatia usafi

WAGANGA na wakunga wa tiba asilia katika Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, wametakiwa kuzingatia usafi wa vifaa wanavyovitumia katika kutoa tiba kwa wananchi, ili kuepuka kueneza magonjwa kutokana na uchafu wa vifaa hivyo. Kauli hiyo, ilitolewa juzi katika Uwanja wa Uhuru na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Zipporah Pangani wakati wa mkutano wa kukabidhi vyeti vya Serikali kwa waganga 13, ambavyo vinawaruhusu kufanya kazi ya kutoa tiba kwa jamii kisheria. Alisema waganga hao wasipozingatia usafi wa vifaa vyao, wanaweza kusababisha kuenea kwa magonjwa kama Ukimwi na kuharisha. Aliwataka waganga kuongeza ujuzi na kuboresha shughuli zao kwa kutumia dawa hizo kutengeneza vidonge na kuitaka jamii kutambua kazi zinazofanywa na waganga hao, maana zipo kwa mujibu wa sheria namba 23 ya mwaka 2002. Naye, Mwenyekiti wa Chama cha Waganga na Wakunga wa Tiba Asilia (STAMATA) Manispaa ya Bukoba, Habibu Mahyoro alisema watu wanaoishi kwa kutegemea viungo vya binadamu si waganga, bali ni matapeli na ni wachawi. Aliiomba Serikali kuwawezesha kupata vitendea kazi, ikiwamo vyombo vya usafiri ambavyo vitatumika kutoa elimu kwa jamii kwa lengo la kupunguza matukio ya wanaojihusisha na matendo maovu ikiwamo mauaji ya albino na vikongwe. Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi katibu wa kamati ya maandalizi, Veidiana Lukeisa alisema waganga wana umuhimu mkubwa, kwani yapo baadhi ya magonjwa ndani ya jamii ambayo hutibiwa na dawa za asili pekee. Aliiomba Serikali kuwashirikisha ili kukabiliana na changamoto mbalimbali, ikiwamo kupambana na magonjwa kama malaria na Ukimwi, kwa kutumia tiba asilia na kutoa ushauri. Aliiomba Serikali kuweka utaratibu utakaosaidia hospitali kuwapokea wagonjwa kutoka kwa waganga na wakunga wa tiba asilia, ili kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika. STAMATA mkoani Kagera, ilianzishwa mwaka 2011 ikiwa na wanachama 47, ambapo sasa ina wanachama 89 kutoka wilaya za Misenyi, Bukoba na
Next Post Previous Post
Bukobawadau