Bukobawadau

Mwigulu Nchemba;Other things Remain Constant

Vijana na watoto wetu ndio tunategemewa kuitumia zaidi katiba mpya. Mabaraza yanaanza, kama wadau nawaomba TUISOME RASIMU, TUTAFAKARI, TUJADILI, TUTOE MAONI KWA KUITANGULIZA TANZANIA MIOYONI MWETU. SIO KULENGA KULIKOMOA KUNDI FULANI AU UPANDE FULANI WA NCHI. Nawashauri tuyaangalie maeneo kwa kina. Kwa kuanzia tuangalie:
A) Ibara ya 223(1) inasema kutakuwa na Jeshi la wananchi wa Tanzania litakalokuwa na mamlaka ya kusimamia ulinzi na usalama.... Ibara ya 232(1) inasema bila kuathiri mashariti ya katiba hii, nchi washarika wa muungano wanaweza kuanzisha vikosi vya ulinzi na usalama .... ktk maeneo yao.
Pili ibara ya 227(1) kutakuwa na Jeshi la Polisi la jamuhuri ya muungano litakuwa na jukumu la ulinzi wa wa watu wao, Ibara ya 232 inaongelea vikosi vya washirika kuhusika na ulinzi wa watu wao
Pia 233 (1) kutakuwa na idara ya usalama wa Taifa wa jamuhuri ya muungano ... Ibara 235 inasema bila kuathiri masharti ya katiba hii, nchi washirika wanaweza kuanzisha idara za usalama.

Analysis, swala la usalama ni nyeti muundo huu utategemea tu mazingira na busara ya viongozi. Vinginevyo nirahisi vikosi vya muungano kupigana na vya nchi washirika kufuatia maelekezo ya viongozi wao siku wakitokea sio wataifa.

B) ibara ya 217(1) kutakuwa na benki kuu ya jamhuri ya muungano na majukumu yameainishwa...... ibara ya 218 serikali washirika zitakuwa na BENKI ZAO zakusimamia sera za kifedha na kibenki
Analysis; hakuna namna unaweza kuwa na monetary policy tatu ktk nchi moja ukafikia malengo. Ni kama gari kuwa na sukani tatu na madreva wa tatu at per, the will miss the right direction.

C) ibara ya 1(1), 1(2) na 57(1) zinazungumzia shirikisho, nionavyo mimi ni makosa. Jamhuri ya muungano ni nchi sio shirikisho. Kupata shirikisho ni sharti kwanza nchi washirika tupige kura kama tunataka kujiunga na shirikisho au laa kama tulivyokataa la afrika mashariki.
Hata muundo wa serikali tatu vijana nawaomba mliangalie kwa utulivu bila jazba ya kelele za ndugu zetu wa upande mwingine kusema wananyonywa pia bila kuangalia mungano wa serikali mbili kuwa ni msimamo wa CCM. TANZANIA BARA ITAKUWA NA SERIKALI MBILI YAANI YA BARA NA YA MUUNGANO ambayo haitahusika na maisha ya watanzania bara kupitia mambo yenye mguso wa moja kwa moja. NITAWALETEA SIKU NYINGINE IMPLICATION ZAKE KIUCHUMI KWA TAKWIMU NA JINSI KODI ITAKAVYOPANDA KUKIDHI NYONGEZA YA SERIKALI.
BE BLESSED
Next Post Previous Post
Bukobawadau