Bukobawadau

TASWIRA MAPOKEZI YA RAIS BARACK OBAMA MCHANA WA LEO

Rais Barack Obama wa nchini Marekani na Mkewe Michelle Obama wakiwa sambamba na watoto zao,wakiwasili  kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere,jijini Dar es Salaam mchana huu kwa ziara ya siku mbili hapa nchini.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Barrack Obama wa Marekani muda mfupi baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mchana wa leo. Kushoto ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe akisalimiana na Mgeni wake Rais wa Marekani,Barack Obama aliewasili nchini Mchana huu kwa ziara ya kikazi ya Siku mbili

Rais Barack Obama akikwagua Gwaride maalum alilioandaliwa akiongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi.
Rais Barack Obama akikwagua Gwaride maalum alilioandaliwa akiongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi. Jenelari Davies Mwamunyange.
Rais wa Marekani Barack Obama akifurahia ngoma za utamaduni mara baada ya kutua nchini Tanzani katika jiji la Dar es salaam

Obama akisalimiana na wananchi kwa furaha.


Rais Barack Obama wa Marekani na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakizungumza na waandishi wa habari, Ikulu 
Next Post Previous Post
Bukobawadau