Bukobawadau

SKYLIGHT BAND JUKWAA MOJA NA DIAMOND PLATINUMZ, LINAH NA RICHIE MAVOKO FIESTA AFTER PARTY NDANI YA GOLD CREST HOTEL JIJINI MWANZA

IMG_8393
Mmiliki wa hoteli ya Gold Crest ya jijini Mwanza ambaye pia ni mchimbaji mdogo wa madini Bw. Mathias Erasto akizungumza machache wakati wa kuikaribisha Skylight Band jijini Mwanza kwenye Fiesta After Party iliyofanyika kwenye hoteli yake mwishoni mwa Juma ambapo pia ameahidi ushirikiano wa karibu sana na Skylight Band na kuwaahidi zaidi wakazi wa Mwanza burudani zaidi kwa kuwaletea wasanii kutoka ndani na nje ya nchi.Kushoto ni Mmiliki wa Skylight Band Dr. Sebastian Ndege a.k.a Jembe ni Jembe
IMG_7814
Aneth Kushaba AK 47 sambamba na Mary Lucos wakitoa burudani kwa wakazi wa Mwanza kwenye After Party ya Fiesta iliyofanyika jijini Mwanza siku ya Jumapili kwenye Hoteli ya Gold Crest.
IMG_7805
Binti mwenye kipaji cha aina yake Mary Lucos akiwapa raha wakazi wa Mwanza.
IMG_7869
Sony Masamba a.k.a Fally Ipupa wa Bongo akitawala jukwaa huku akipewa sapoti na Mary Lucos pamoja na Digna ndani ya Gold Crest Hotel.
IMG_7879
Sehemu ya umati wa wakazi wa Mwanza waliojitokeza kushuhudia burudani ya Skylight Band.
IMG_7970
Aneth Kushaba AK47 akifanya yake ukumbini.
IMG_7990
Aneth Kushaba AK 47 akimpagawisha shabiki wake katika ukumbi wa Hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza.
IMG_8053
Ebwana hii Band ni noma aisee...Wadau wakiwa VIP wakiangalia burudani ya Skylight Band na hawakuamini macho yao.
IMG_8063
Hapana Chezea Skylight Band wewe....
IMG_8457
Mmiliki wa hoteli ya Gold Crest ya jijini Mwanza ambaye pia ni mchimbaji mdogo wa madini Bw. Mathias Erasto akionyesha umahiri wake wa kusakata sebene la Skylight Band ndani ya ukumbi wa Hoteli hiyo.
IMG_8320
Shabiki wa kizungu na mdau wa jijini Mwanza wakionekana kuchizika na Skylight Band.
IMG_8490
Msanii Diamond Platinumz akiingia ukumbi kupiga show jukwaa moja na Skylight Band kwa mara ya kwanza kuimba na Live Band jijini Mwanza.
IMG_8498
Wakazi wa jiji la Mwanza wakimshangilia Diamond alipokuwa akiingia ukumbini huku wengine wakimpiga picha.
IMG_8668
Msanii nyota wa Bongo Flava Diamond Platinumz akitoa burudani kwa wakazi wa Mwanza kwenye Fiesta After Party na Live Band ya Skylight. Kulia ni Sam Mapenzi wa Skylight Band wakiimba pamoja na Diamond.
IMG_8503
IMG_8681
Diamond Platinumz akiwacheza mashabiki wake wa Mwanza Style ya Ngolongolo kwenye wimbo wake mpya unaobamba na kufahamika kwa jina la "My Number One".
IMG_8688
Diamond Platinumz akicheza style yake ya Ngololo na mashabiki wake wa Mwanza ndani ya Gold Crest Hotel.
IMG_8661
Wengine walipanda jukwaani na kupiga nae picha za ukumbusho.
IMG_8529
Ukumbi ulifurika ni balaaa....
IMG_8496
IMG_8116
Msanii wa muziki nchini Linah Sanga akitoa burudani kwenye Fiesta After Party sambamba na Mary Lucos wa Skylight Band ndani ya Gold Crest Hotel.
IMG_8126
Linah akicheza na mashabiki wake wa jijini Mwanza.
IMG_8157
Linah ft Sam Mapenzi wa Skylight Band wakitoa burudani kwenye Fiesta After Party iliyofanyika mwishoni mwa Juma ndani ya Gold Crest Hotel.
IMG_8176
Msanii Richie Mavoko na Skylight Band wakipagawisha wakazi wa Mwanza.
IMG_7993
Wakazi wa jijini Mwanza wakinywa na kufurahi huku burudani ya Skylight Band ikiendelea.
IMG_8354
Warembo wa Ukweeee walipamba ukumbi wa hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza wakati wa Fiesta After Party jijini Mwanza.
IMG_8390
IMG_7883
Wengine wakiwa wamekaa kwenye kushuhudia burudani ya kukata na shoka iliyokuwa ikitolewa na Skylight Band.
IMG_8000
Jukwaa la Skylight Band lilipambwa na Richi Mavoko pamoja na Linah kama wanavyoonekana Back Stage na Sam Mapenzi wa Skylight Band.
IMG_8022
Palikuwa hapatoshi Gold Crest Hoteli.
IMG_8026
IMG_8327
Wadau wa Mwanza wakishow love mbele ya camera yetu.
IMG_8295
Yachuma mimi nataka mukanda ya chuma chuma....Style mpya ya Skylight Band inayofahamika kama Yachuma chuma.
Next Post Previous Post
Bukobawadau